1 Hapo Yobu akajibu:
2 “Mambo kama hayo nimeyasikia mengi;nyinyi ni wafariji duni kabisa!
3 Mwisho wa maneno haya matupu ni lini?Au ni kitu gani kinachowachochea kujibu?
4 Kama nyinyi mngekuwa mimi, na mimi nyinyi,ningeweza kusema kama nyinyiningeweza kubuni maneno dhidi yenu,na kutikisa kichwa changu.
5 Ningeweza kuwatia moyo kwa maneno yangu,na maneno yangu ya faraja yangewatuliza.
6 “Lakini nikisema maumivu yangu hayatulii,na nikikaa kimya hayaondoki.
7 Kweli Mungu amenichakazaameharibu kila kitu karibu nami.
8 Amenifanya ninyauke, na huo ni ushindi dhidi yangu.Kukonda kwangu kumenikabilina kushuhudia dhidi yangu.
9 Amenirarua kwa hasira na kunichukia;amenisagia meno;na adui yangu ananikodolea macho.
10 Watu wananidhihaki na kunicheka;makundi kwa makundi hunizunguka,na kunipiga makofi mashavuni.
11 Mungu amenitia mikononi mwa wajeuri,na kunitupa mikononi mwa waovu.
12 Nilikuwa nimestarehe, lakini akanivunjavunja,alinikaba shingo na kunipasua vipandevipande;alinifanya shabaha ya mishale yake,
13 akanipiga mishale kutoka kila upande.Amenipasua figo bila huruma,na nyongo yangu akaimwaga chini.
14 Hunivunja na kunipiga tena na tena;hunishambulia kama askari.
15 “Nimejishonea mavazi ya gunia,fahari yangu nimeibwaga mavumbini.
16 Uso wangu ni mwekundu kwa kulia,kope zangu zimekuwa nyeusi ti;
17 ingawa sijafanya dhuluma kwa mkono wangu,na sala zangu kwa Mungu ni safi.
18 “Ewe dunia, usiifunike damu yangu iliyomwagika;kilio changu kienee kila mahali.
19 Nina hakika ninaye shahidi wangu mbinguni,mwenye kunitetea yuko huko juu.
20 Rafiki zangu wanidharau;nabubujika machozi kumwomba Mungu.
21 Laiti mtu angenitetea mbele ya Mungu,kama ifanyikavyo duniani kati za watu wawili.
22 Naam, miaka yangu ni michache,nami nitakwenda huko ambako sitarudi.