1 “Nimevunjika moyo, siku zangu zimekwisha,kaburi langu liko tayari.
2 Kweli wanaonidhihaki wamenizunguka,dhihaka zao naziona dhahiri.
3 “Ee Mungu, uwe mdhamini wangu mbele yako,maana hakuna mwingine wa kunidhamini.
4 Maadamu umezifumba akili za rafiki zangu;usiwaache basi wanishinde.