4 Maadamu umezifumba akili za rafiki zangu;usiwaache basi wanishinde.
5 Mtu anayewasaliti rafiki zake kwa faidawatoto wake watakufa macho.
6 “Nimefanywa kuwa kichekesho kwa watunimekuwa mtu wa kutemewa mate.
7 Macho yangu yamefifia kwa uchungu;viungo vyangu vyote vimekuwa kama kivuli.
8 Wanyofu wanaduwaa waonapo balaa langu,nao wasio na hatia hujichocheadhidi ya mtu wanayedhani hamchi Mungu.
9 Hata hivyo, mnyofu hushikilia msimamo wake,mtu atendaye mema huzidi kuwa na nguvu zaidi.
10 Lakini nyinyi njoni, njoni nyote tena,kwenu sitampata mwenye hekima hata mmoja.