14 Anangolewa katika nyumba aliyoitegemea,na kupelekwa kwa mfalme wa vitisho.
15 Nyumba yake tupu, wengine wataishi humo;madini ya kiberiti yametawanywa katika makao yake.
16 Yeye ni kama mti uliokauka mizizi,matawi yake juu yamenyauka.
17 Nchini hakuna atakayemkumbuka;jina lake halitatamkwa tena barabarani.
18 Ameondolewa mwangani akatupwa gizani;amefukuzwa mbali kutoka duniani.
19 Hana watoto wala wajukuu;hakuna aliyesalia katika makao yake.
20 Watu wa magharibi wameshangazwa na yaliyompata,hofu imewakumba watu wa mashariki.