3 Kwa nini unatufanya kama ng'ombe?Mbona unatuona sisi kuwa wapumbavu?
4 Wewe unajirarua mwenyewe kwa hasira zako.Kwani, dunia itaachwa tupu kwa ajili yakoau miamba ihamishwe toka mahali pake?
5 “Naam, mwanga wa mtu mwovu utazimishwa;mwali wa moto wake hautangaa.
6 Nyumbani kwake mwanga ni giza,taa inayomwangazia itazimwa.
7 Hatua zake ndefu zitafupishwa;mipango yake itamwangusha chini.
8 Nyayo zake mwenyewe zitamtia mtegoni;kila akitembea anakumbana na shimo.
9 Mtego humkamata kisiginoni,tanzi humbana kabisa.