11 Ameichochea ghadhabu yake dhidi yangu;ameniona kuwa kama adui yake.
12 Majeshi yake yanijia kwa pamoja;yametengeneza njia ya kuja kwangu,yamepiga kambi kuizunguka nyumba yangu.
13 Mungu amewaweka ndugu zangu mbali nami;rafiki zangu wakuu wamenitoroka kabisa.
14 Jamaa zangu na marafiki hawanisaidii tena.
15 Wageni nyumbani mwangu wamenisahau;watumishi wangu wa kike waniona kuwa mgeni.Mimi nimekuwa kwao mtu wasiyemjua.
16 Namwita mtumishi wangu lakini haitikii,ninalazimika kumsihi sana kwa maneno.
17 Nimekuwa kinyaa kwa mke wangu;chukizo kwa ndugu zangu mwenyewe.