5 Mnaishusha hadhi yangu mpate kujikuza;mnanilaumu kwa kunyenyekezwa kwangu.
6 Jueni kwamba Mungu amenitendea vibaya,na kuninasa katika wavu wake.
7 Tazama napiga yowe: ‘Dhuluma!’Lakini sijibiwi.Naita kwa sauti kubwa,lakini sipati haki yangu.
8 Njia yangu ameiziba kwa ukuta ili nisipiteamezitia giza njia zangu.
9 Amenivua fahari yangu;ameiondoa taji yangu kichwani.
10 Amenivunja pande zote, nami nimekwisha;tumaini langu amelingoa kama mti.
11 Ameichochea ghadhabu yake dhidi yangu;ameniona kuwa kama adui yake.