15 “Je, umeamua kufuata njia za zamaniambazo watu waovu wamezifuata?
16 Hao walifagiliwa kabla ya wakati wao,misingi yao ilikumbwa mbali na maji.
17 Hao ndio waliomwambia Mungu, ‘Achana nasi!’Na ‘Wewe Mungu Mwenye Nguvu waweza nini juu yetu?’
18 Lakini Mungu ndiye aliyejaza nyumba zao fanaka,lakini walimweka mbali na mipango yao!
19 Wanyofu huona na kufurahi,wasio na hatia huwacheka na kuwadharau,
20 Wanasema ama kweli maadui zetu wameangamizwa,na walichobakiza kimeteketezwa kwa moto.
21 “Sasa, Yobu, kubaliana na Mungu uwe na amani,na hapo mema yatakujia.