10 Lakini yeye anajua njia ninayofuata;atakapomaliza kunijaribunitatoka humo safi kama dhahabu.
11 Nafuata nyayo zake kwa uaminifunjia yake nimeishikilia wala sikupinda.
12 Kamwe sijaacha kushika amri yake,maneno yake nimeyatunza moyoni mwangu.
13 Lakini yeye habadiliki, nani awezaye kumgeuza?Analotaka, ndilo analofanya!
14 Atanijulisha yote aliyonipangia;na mengi kama hayo yamo akilini mwake.
15 Hivyo, natetemeka kwa hofu mbele yake;hata nikifikiria tu napatwa na woga.
16 Mungu ameufanya moyo wangu ufifie,Mungu Mwenye Nguvu amenitia hofu.