13 Lakini yeye habadiliki, nani awezaye kumgeuza?Analotaka, ndilo analofanya!
14 Atanijulisha yote aliyonipangia;na mengi kama hayo yamo akilini mwake.
15 Hivyo, natetemeka kwa hofu mbele yake;hata nikifikiria tu napatwa na woga.
16 Mungu ameufanya moyo wangu ufifie,Mungu Mwenye Nguvu amenitia hofu.
17 Maana nimekumbwa na giza,na giza nene limetanda usoni mwangu.