7 Mungu hutandaza kaskazini mahali patupu,na hutundika dunia mahali pasipo na kitu,
8 huyafunga maji mawinguni yawe mazito,nayo mawingu hayapasuki kwa uzito wake.
9 Huufunika uso wa mwezina kutandaza juu yake wingu.
10 Amechora duara juu ya uso wa bahari,penye mpaka kati ya mwanga na giza.
11 Mungu akitoa sauti ya kukemea,nguzo za mbingu hutetemeka na kustaajabu.
12 Kwa nguvu zake aliituliza bahari;kwa maarifa yake alimwangamiza dude Rahabu.
13 Kwa pumzi yake aliisafisha anga;mkono wake ulilichoma joka lirukalo.