20 Vitisho humvamia kama mafuriko;usiku hukumbwa na kimbunga.
21 Upepo wa mashariki humpeperusha akatoweka;humfagilia mbali kutoka makao yake.
22 Upepo huo humvamia bila huruma;atajaribu kuukimbia lakini mbio za bure.
23 Upepo humzomea akimbiapo,na kumfyonya toka mahali pake.