5 Siwezi kabisa kusema kuwa nyinyi mnasema ukwelimpaka kufa kwangu nasema sina hatia.
6 Nashikilia unyofu wangu, wala sitauacha;katika dhamiri yangu sina cha kunihukumu maishani mwangu.
7 “Adui yangu na apate adhabu ya mwovu,anayeinuka kunilaumu aadhibiwe kama mbaya.
8 Asiyemcha Mungu ana tumaini gani,Mungu anapomkatilia mbali,anapomwondolea uhai wake?
9 Je, atakapokumbwa na taabu,Mungu atasikia kilio chake?
10 Mwovu hawezi kufurahi mbele ya Mungu Mwenye Nguvu;hataweza kudumu akimwomba Mungu.
11 Nitawafundisheni kitendo cha Mungu kilivyo,sitawaficheni mipango yake Mungu Mwenye Nguvu.