17 Nilizivunja nguvu za watu waovu,nikawafanya wawaachilie mateka wao.
18 Kisha nikafikiri: Nitafia kiotani mwangu nimetulia;siku za maisha yangu zitaongezeka kama mchanga.
19 Mimi ni kama mti uliotandaza mizizi majini,umande wa usiku huburudisha matawi yangu.
20 Napata fahari mpya daima,na nguvu zangu tayari kama mshale na upinde.
21 “Wakati huo watu walinisikiliza na kungoja,walikaa kimya kungojea shauri langu.
22 Nilipomaliza kusema hawakuwa na cha kuongeza,maneno yangu yaliwakolea kama matone ya mvua.
23 Watu waliningojea kama wangojeavyo mvua,walikuwa kama watu wanaotazamia msimu wa vuli.