15 ningekuwa pamoja na wakuu waliokuwa na dhahabu,waliojaza nyumba zao fedha tele.
16 Au, mbona sikuwa kama mimba iliyoharibika,naam, kama mtoto aliyezaliwa mfu?
17 Huko kwa wafu waovu hawamsumbui mtu,huko wachovu hupumzika.
18 Huko wafungwa hustarehe pamoja,hawaisikii kamwe sauti ya mnyapara.
19 Wakubwa na wadogo wako huko,nao watumwa wamepata uhuru mbali na bwana zao.
20 Ya nini kumjalia nuru yule aliye taabuni;na uhai yule aliye na huzuni moyoni?
21 Mtu atamaniye kifo lakini hafi;hutafuta kifo kuliko hazina iliyofichika.