1 Kisha Elihu akaendelea kusema:
2 “Sikilizeni maneno yangu enyi wenye hekima,nitegeeni masikio yenu, nyinyi wenye ujuzi.
3 Sikio huyapima maneno,kama vile ulimi uonjavyo chakula.
4 Basi, na tuchague lililo sawa,tuamue miongoni mwetu lililo jema.