19 Tufundishe tutakachomwambia Mungu;maana hoja zetu si wazi, tumo gizani.
20 Je, nani anathubutu kumwambia: Nataka kuongea?Nani aseme apate balaa?
21 “Ghafla mtu hawezi tena kuona waziwazi:Jua limefichika nyuma ya mawingu,na upepo umefagia anga!
22 Mngao mzuri hutokea kaskazini;Mungu amezungukwa na utukufu wa kutisha.
23 Mungu Mwenye Nguvu asiyeweza kufikiwa na mtu,uwezo na uadilifu wake ni mkuu,amejaa wema wala hapotoshi haki kamwe.
24 Kwa hiyo, watu wote humwogopa;yeye hamjali mtu yeyote mwenye kiburi.”