3 Huufanya uenee chini ya mbingu yote,umeme wake huueneza pembe zote za dunia.
4 Ndipo sauti yake hunguruma,sauti ya Mungu hunguruma kwa faharina muda huo wote umeme humulikamulika.
5 Mungu hupiga radi ya ajabu kwa sauti yake,hufanya mambo makuu tusiyoweza kuyaelewa.
6 Huiambia theluji, ‘Anguka juu ya nchi!’Na manyunyu na mvua, ‘Nyesha kwa nguvu.’
7 Hufunga shughuli za kila mtu;ili watu wote watambue kazi yake.
8 Wanyama wa porini hurudi mafichoni mwao,na hubaki katika mapango yao.
9 Dhoruba huvuma kutoka chumba chake,na baridi kali kutoka ghalani mwake.