15 Lakini waovu watanyimwa mwanga wao,mkono wanaonyosha kupiga watu utavunjwa.
16 “Je, umepata kufika kwenye chemchemi za bahari?au kutembea juu ya sakafu ya kilindi cha bahari?
17 Je, umewahi kuoneshwa malango ya kifo,au kuyaona malango ya makazi ya giza nene?
18 Je, wajua ukubwa wa dunia?Niambie kama unajua haya yote.
19 “Je, makao ya mwanga yako wapi?Nyumbani kwa giza ni wapi,
20 ili upate kulipeleka kwenye makao yake,na kuifahamu njia ya kwenda huko kwake.
21 Wewe unapaswa kujua,wewe ambaye umekwisha ishi miaka mingi!