24 Ipi njia ya kwenda mahali mwanga unapogawanywa,au huko kunakotoka upepo wa mashariki ukasambazwa duniani?
25 “Nani aliyechora angani njia kwa ajili ya mvua?Nani aliyeionesha radi njia yake mawinguni,
26 ikasababisha mvua kunyesha nchini kusikoishi mtuna jangwani ambako hakuna mtu,
27 ili kuiburudisha nchi kavu na kamena kuifanya iote nyasi?
28 “Je, mvua ina baba?Au nani ameyazaa matone ya umande?
29 Je, barafu ilitoka tumboni kwa nani?Nani aliyeizaa theluji?
30 Maji hugeuka kuwa magumu kama jiwe,na uso wa bahari ukaganda.