6 Je, nguzo za dunia zimesimikwa juu ya nini,au nani aliyeliweka jiwe lake la msingi,
7 nyota za asubuhi zilipokuwa zikiimba pamoja,na wana wa Mungu wakapaza sauti za shangwe?
8 Ni nani aliyeyafunga mafuriko ya bahariwakati yalipozuka na kuvuma kutoka vilindini?
9 Mimi ndiye niliyeifunika bahari kwa mawinguna kuiviringishia giza nene.
10 Niliiwekea bahari mipaka,nikaizuia kwa makomeo na milango,
11 nikaiambia: ‘Mwisho wako ni hapa, si zaidi!Mawimbi yako ya nguvu yatakomea hapa!’
12 “Yobu, tangu uzaliwe umewahi kuamuru kupambazuke?na kulifanya pambazuko lijue mahali pake,