9 Mimi ndiye niliyeifunika bahari kwa mawinguna kuiviringishia giza nene.
10 Niliiwekea bahari mipaka,nikaizuia kwa makomeo na milango,
11 nikaiambia: ‘Mwisho wako ni hapa, si zaidi!Mawimbi yako ya nguvu yatakomea hapa!’
12 “Yobu, tangu uzaliwe umewahi kuamuru kupambazuke?na kulifanya pambazuko lijue mahali pake,
13 ili lipate kuikamata dunia kwa pembe zakena kuwatimulia mbali waovu waliomo?
14 Dunia hugeuka na kupata rangi kama vazi;kama udongo wa mfinyanzi unavyogeuzwa na mhuri.
15 Lakini waovu watanyimwa mwanga wao,mkono wanaonyosha kupiga watu utavunjwa.