8 Je, unataka kweli kubatilisha hukumu yangu,kuniona nina hatia ili wewe usiwe na hatia?
9 Je, una nguvu kama mimi Mungu?Waweza kunguruma kwa sauti kama yangu?
10 “Basi, jioneshe kuwa na fahari na ukuu,ujipambe kwa utukufu na fahari.
11 Wamwagie watu hasira yako kuu;mwangalie kila mwenye kiburi na kumwangusha.
12 Mwangalie kila mwenye kiburi na kumporomosha,uwakanyage waovu mahali walipo.
13 Wazike wote pamoja ardhini;mfunge kila mmoja kwa kifungo cha kifo.
14 Hapo nitakutambua,kwamba nguvu yako mwenyewe imekupa ushindi.