1 Kisha Yobu akamjibu Mwenyezi-Mungu:
2 “Najua kwamba waweza kila kitu,lolote unalokusudia haliwezi kuzuiliwa.
3 Ulisema kuwa nilithubutu kutatiza mpango wako kijinga.Kweli nilitamka kitu ambacho sikuelewamambo ya ajabu mno kwanguambayo sikuwa ninayajua.
4 Uliniambia nisikilize nawe utaniambia;kwamba utaniuliza nami nikujibu.
5 Kweli nilikuwa nimesikia habari zako kwa masikio tu,lakini sasa nakuona kwa macho yangu mwenyewe.
6 Kwa hiyo natubu pamoja na kujipaka mavumbi na majivu,najiona mimi mwenyewe kuwa si kitu kabisa.”
7 Mwenyezi-Mungu alipomaliza kuongea na Yobu, alimwambia Elifazi, Mtemani, “Ghadhabu yangu imewaka dhidi yako na marafiki zako wawili kwani hamkusema ukweli juu yangu kama mtumishi wangu Yobu alivyofanya.