4 Kama watoto wako wamemkosea Mungu,yeye amewalipiza matokeo ya uhalifu wao.
5 Kama utamtafuta Munguukamsihi huyo Mungu mwenye nguvu,
6 kama wewe u safi moyoni na mnyofu,kweli Mungu atakuja kukusaidia,na kukujalia makao unayostahili.
7 Na ingawa ulianza kuishi kwa unyongemaisha yako ya baadaye yatakuwa ya fahari zaidi.
8 Jifunze tafadhali kwa wale waliotutangulia,zingatia mambo waliyogundua hao wazee.
9 Sisi ni watu wa juzijuzi tu, hatujui kitu;siku zetu duniani ni kivuli kipitacho.
10 Lakini wao watakufunza na kukuambia,mambo waliyopata kuyatoa katika maarifa yao: