1 Hatimaye Yobu aliamua kuongea, akailaani siku aliyozaliwa.
2 Yobu akasema:
3 “Ilaaniwe siku ile niliyozaliwa;usiku ule iliposemwa, ‘Mwana amechukuliwa mimba’
4 Siku hiyo na iwe giza!Mungu juu asijishughulishe nayo!Wala nuru yoyote isiiangaze!
5 Mauzauza na giza nene yaikumbe,mawingu mazito yaifunike.Giza la mchana liitishe!