5 Upanga wa Mungu uko tayari juu mbinguni.Tazama, washuka kuwaadhibu Waedomu,watu ambao ameamua kuwaangamiza.
6 Upanga utalowa damu na kutapakaa mafuta,kama kwa damu ya kondoo na mbuzi,na mafuta ya figo za kondoo dume.Maana Mwenyezi-Mungu atatoa kafara huko Bosra,kutakuwa na mauaji makubwa nchini Edomu.
7 Nyati wataangamia pamoja nao,ndama kadhalika na mafahali.Nchi italoweshwa damu,udongo utarutubika kwa mafuta yao.
8 Maana Mwenyezi-Mungu anayo siku ya kisasi;mwaka wa kulipiza maadui wa Siyoni.
9 Vijito vya Edomu vitatiririka lami,udongo wake utakuwa madini ya kiberiti;ardhi yake itakuwa lami iwakayo.
10 Itawaka usiku na mchana bila kuzimika,moshi wake utafuka juu milele.Nchi itakuwa jangwa siku zote,hakuna atakayepitia huko milele.
11 Itakuwa makao ya kozi na nungunungu,bundi na kunguru wataishi humo.Mwenyezi-Mungu atawaletea ghasia,na timazi la fujo kwa wakuu wake.