5 Maadui za watu wangu wakitaka ulinzi wangu,basi, na wafanye amani nami;naam, wafanye amani nami.”
6 Itakuja siku wazawa wa Yakobo watashika mizizi;naam, watu wa Israeli watachanua na kuchipua,na kuijaza dunia yote kwa matunda.
7 Mungu hakuwaadhibu Waisraeli vikalikama alivyowaadhibu maadui wake;Waisraeli waliopotea vitani,ni wachache kuliko wale wa maadui zake.
8 Aliwaadhibu watu wake kwa kuwapeleka uhamishoni.Wakati wa upepo mkali wa mashariki,aliwaondoa kwa kipigo kikali.
9 Hivi ndivyo uovu wa wazawa wa Yakobo utakavyoondolewa,hivi ndivyo dhambi yake itakavyofutwa kabisa:Ataziharibu madhabahu za miungu;mawe yake yatasagwasagwa kama chokaa;Ashera, wala madhabahu za kufukizia ubani hazitabaki.
10 Mji ule wa ngome sasa umekuwa mtupu,umeachwa na kuhamwa kama jangwa,humo ndama wanalisha na kupumzika.
11 Matawi ya miti yamekauka na kuvunjika;kina mama huyaokota wakawashia moto.Watu hawa hawajaelewa kitu,kwa hiyo Mungu, Muumba wao, hatawahurumia,yeye aliyewafanya, hatawafadhili.