2 Bila kunitaka shauri, wanafunga safari kwenda Misri,kukimbilia usalama katika ulinzi wa Farao,kupata mahali pa usalama nchini Misri.
3 Lakini ulinzi wa Farao utakuwa aibu yenu,na usalama nchini Misri utakuwa fedheha yenu.
4 Maana ingawa maofisa wao wamefika Soani,na wajumbe wao mpaka Hanesi,
5 wote wataaibishwa na hao wasioweza kuwasaidia,watu ambao hawawezi kuwapa msaada au faida,ila tu kuwapa aibu na fedheha.”
6 Kauli ya Mungu juu ya wanyama wa pande za Negebu:“Wajumbe wanapita katika nchi ya taabu na shida,yenye simba, nyoka wa sumu na majoka.Wamewabebesha wanyama wao mali zao,kuwapelekea watu wasioweza kuwafaa kitu.
7 Maana msaada wa Misri ni bure, haufai kitu;kwa hiyo nimeipanga Misri jina:‘Joka lisilo na nguvu!’”
8 Mungu aliniambia:“Sasa chukua kibao cha kuandikia,uandike jambo hili mbele yao,liwe ushahidi wa milele: