11 Ole wao wanaoamka asubuhi na mapemawapate kukimbilia kunywa kileo;wanaokesha hata usiku,mpaka divai iwaleweshe!
12 Katika karamu zao, hapakosekani vinubi,zeze, matari, filimbi na divai.Lakini hawajali matendo ya Mwenyezi-Mungu,wala kuzitambua kazi za mikono yake.
13 Kwa hiyo, watu wangu watapelekwa uhamishonikwa sababu ya utovu wao wa akili.Watu wenu mashuhuri watakufa njaa,watu wengi watakufa kwa kiu.
14 Kuzimu inawangoja kwa hamu kubwa,imepanua kinywa chake mpaka mwisho.Waheshimiwa pamoja na raia wa Yerusalemuwanaingia humo makundi kwa makundi,kadhalika na wote wanaousherehekea.
15 Kila mtu atafedheheshwa,na wenye kiburi wote wataaibishwa.
16 Lakini Mwenyezi-Mungu wa majeshi atatukuzwa.Yeye huonesha ukuu wakekwa matendo yake ya haki,kwa kuwahukumu watu wake.
17 Wanakondoo, wanambuzi na ndama,watapata malisho yao kwenye magofu ya miji yao,kana kwamba hizo ni sehemu za malisho yao.