7 Je, huu ndio mji wa furaha wa Tiro,mji ambao ulijengwa zamani za kale,ambao wakazi wake walikwenda kumiliki nchi za mbali?
8 Ni nani aliyepanga mambo haya dhidi ya Tiro,mji uliowatawaza wafalme,wafanyabiashara wake walikuwa wakuu,wakaheshimiwa duniani kote?
9 Ni Mwenyezi-Mungu wa majeshi!Yeye ndiye aliyeyapanga haya yote.Alifanya hivyo akiharibu kiburi chaona kuwaaibisha waheshimiwa wake.
10 Limeni sasa ardhi yenu enyi wakazi wa Tarshishi;maana hamna tena bandari kwa ajili ya meli kubwa.
11 Mwenyezi-Mungu ameunyosha mkono wake juu ya bahari,amezitetemesha falme;ametoa amri kuziharibu ngome za Kanaani.
12 Alisema: “Ewe binti Sidonihutaweza kufanya sherehe tena;hata ukikimbilia Kupro,huko nako hutapata pumziko!”
13 (Ni Wakaldayo, wala si Waashuru, waliowaacha wanyama wa porini wauvamie mji wa Tiro. Wao ndio waliouzungushia mji huo minara ya kuushambulia, wakayabomoa majumba yake na kuufanya magofu.)