12 Watu wangu watarudi kutoka mbali,wengine kutoka kaskazini na magharibi,wengine kutoka upande wa kusini.”
13 Imbeni kwa furaha, enyi mbingu!Shangilia ewe dunia.Pazeni sauti mwimbe enyi milima,maana Mwenyezi-Mungu amewafariji watu wake,naam, atawaonea huruma watu wake wanaoteseka.
14 Wewe Siyoni wasema:“Mwenyezi-Mungu ameniacha;hakika Bwana wangu amenisahau.”
15 Lakini Mwenyezi-Mungu asema:“Je, mama aweza kumsahau mwanawe anayenyonya,asimwonee huruma mtoto wa tumbo lake?Hata kama mama aweza kumsahau mwanawe,mimi kamwe sitakusahau.
16 Nimekuchora katika viganja vyangu;kuta zako naziona daima mbele yangu.
17 Watakaokujenga upya wanakuja haraka,wale waliokuharibu wanaondoka.
18 Inua macho uangalie pande zote;watu wako wote wanakusanyika na kukujia.Naapa kwa nafsi yangu mimi Mwenyezi-Mungu,watu wako watakuwa kwako kama mapambo,utawafurahia kama afanyavyo bibi arusi na utaji wake.