1 Nitaimba juu ya rafiki yangu,wimbo wa rafiki yangu na shamba lake la mizabibu:Rafiki yangu alikuwa na shamba la mizabibujuu ya kilima chenye rutuba nyingi.
2 Alililima vizuri na kuondoa mawe yote,akaotesha humo mizabibu iliyochaguliwa;alijenga mnara wa ulinzi katikati yake,akachimba kisima cha kusindikia divai.Kisha akangojea lizae zabibu,lakini likazaa zabibu chungu.
3 Kwa hiyo rafiki yangu anasema hivi:“Enyi wakazi wa Yerusalemu na watu wa Yuda,amueni tafadhali kati yangu na shamba langu.
4 Ni kitu gani nilichokosa kulifanyia shamba langu?Na nilipotazamia lizae zabibu nzuri,mbona basi, likazaa zabibu chungu?
5 “Na sasa nitawaambieninitakavyolifanya hilo shamba langu.Nitauondoa ua wake,nalo litaharibiwa.Nitaubomoa ukuta wake,nalo litakanyagwakanyagwa.