18 Ole wao wanaoburuta uovu kama kwa kamba;wanaokokota dhambi kama kwa kamba za mkokoteni.
19 Wanasema:“Mwache Mwenyezi-Mungu afanye haraka,tunataka kuyaona aliyosema atayafanya!Mtakatifu wa Israeli na atimize kusudi lake.Hebu na tuone ana mipango gani!”
20 Ole wao wanaosema uovu ni wemana wema ni uovu.Giza wanasema ni mwangana mwanga wanasema ni giza.Kichungu wanasema ni kitamuna kitamu wanakiona kuwa kichungu.
21 Ole wao wanaojiona kuwa wenye hekimaambao wanajiona kuwa wenye akili.
22 Ole wao mabingwa wa kunywa divai,hodari sana wa kuchanganya vileo.
23 Kwa hongo kidogo wanawaachilia wenye hatiana kuwanyima wasio na hatia haki yao.
24 Kwa hiyo, kama moto uteketezavyo nyasi,kama majani yateketeavyo katika mwali wa motondivyo na mizizi yao itakavyooza,na maua yao yatakavyopeperushwa juu kama vumbi.Maana wameiacha sheria ya Mwenyezi-Mungu wa majeshi,wamedharau neno la yule Mtakatifu wa Israeli.