4 Ni kitu gani nilichokosa kulifanyia shamba langu?Na nilipotazamia lizae zabibu nzuri,mbona basi, likazaa zabibu chungu?
5 “Na sasa nitawaambieninitakavyolifanya hilo shamba langu.Nitauondoa ua wake,nalo litaharibiwa.Nitaubomoa ukuta wake,nalo litakanyagwakanyagwa.
6 Nitaliacha liharibiwe kabisa,mizabibu yake haitapogolewa wala kupaliliwa.Litaota mbigili na miiba.Tena nitayaamuru mawinguyasinyeshe mvua juu yake.”
7 Naam! Shamba la mizabibu la Mwenyezi-Mungu wa majeshini jumuiya ya Waisraeli,na mizabibu mizuri aliyoipanda ni watu wa Yuda.Yeye alitazamia watende haki,badala yake wakafanya mauaji;alitazamia uadilifu,badala yake wakasababisha kilio!
8 Ole wao wanaonunua nyumba baada ya nyumba,wanaoongeza mashamba juu ya mashamba yao,mpaka kila sehemu inakuwa mali yao,na hamna nafasi kwa wengine nchini.
9 Nimemsikia Mwenyezi-Mungu wa majeshi akitamka hivi:“Hakika nyumba nyingi zitabaki tupu,majumba makubwa mazuri bila wakazi.
10 Shamba la mizabibu la eka kumilitatoa lita nane tu za divai;anayepanda kilo 100 za mbeguatavuna kilo 10 tu za nafaka.”