3 niwape wale wanaoomboleza katika Siyonitaji la maua badala ya majivu,mafuta ya furaha badala ya maombolezo,vazi la sifa badala ya moyo mzito.Nao wataitwa mialoni madhubuti,aliyopanda Mwenyezi-Mungu kuonesha utukufu wake.
4 Watayajenga upya magofu ya zamani,wataisimika miji iliyoharibiwa hapo kwanza;wataitengeneza miji iliyobomolewa,uharibifu wa vizazi vingi vilivyopita.
5 Wageni watakuwa hapo kuwachungia mifugo yenu;watawalimia na kuwatunzia mizabibu yenu.
6 Nanyi mtaitwa: “Makuhani wa Mwenyezi-Mungu”,Mtaitwa: “Watumishi wake Mungu wetu”.Mtafaidika kwa utajiri wa mataifa,mtatukuka kwa mali zao.
7 Kwa vile mlipata aibu maradufu,watu wakaona kuwa fedheha ni majaliwa yenu,sasa mtapata eneo maradufu kuwa mali yenu,na furaha yenu itadumu milele.
8 “Mimi Mwenyezi-Mungu napenda haki;nachukia unyanganyi na uhalifu.Nitawatuza watu wangu kwa uaminifu,nitafanya nao agano la milele.
9 Wazawa wao watakuwa maarufu kati ya mataifa;watajulikana kuwa maarufu kati ya watu wengine.Kila atakayewaona atakiri kwambawao ni watu aliowabariki Mwenyezi-Mungu.”