1 Ni nani huyu ajaye kutoka Edomu,anayefika kutoka Bosra na mavazi ya madoa mekundu?Ni nani huyo aliyevaa mavazi ya fahari,anatembea kwa nguvu zake kubwa?Ni mimi Mwenyezi-Munguninayetangaza ushindi wangu;nami ni mwenye nguvu ya kuokoa.
2 Lakini mbona nguo yako ni nyekundu,nyekundu kama ya mtu anayekamua zabibu?
3 “Naam, nimekamua zabibu peke yangu,wala hakuna mtu aliyekuja kunisaidia.Nimeyakanyaga mataifa kwa hasira yangu,niliyapondaponda kwa ghadhabu yangu.Nguo zangu zimejaa madoa ya damu yao,imeyachafua kabisa mavazi yangu.
4 Niliamua kuwa siku ya kulipiza kisasi imefika;wakati wa kuwakomboa watu wangu umefika.
5 Nilitazama na hapakuwa na wa kunisaidia;nilishangaa hapakuwa na wa kuniunga mkono.Lakini nilijipatia ushindi kwa mkono wangu,ghadhabu yangu ilinihimiza.
6 Kwa hasira yangu niliwaponda watu,niliwalewesha kwa ghadhabu yangu;damu yao niliimwaga chini ardhini.”