14 Pigeni yowe enyi meli za Tarshishi,maana kimbilio lenu limeharibiwa.
15 Hapo mji wa Tiro utasahaulika kwa muda wa miaka sabini, muda wa maisha ya mfalme. Baada ya miaka hiyo sabini, mji wa Tiro utakumbwa na kile watu wanachoimba juu ya malaya:
16 “Twaa kinubi chakouzungukezunguke mjini,ewe malaya uliyesahaulika!Imba nyimbo tamutamu.Imba nyimbo nyinginyingiili upate kukumbukwa tena.”
17 Baada ya miaka hiyo sabini, Mwenyezi-Mungu atauadhibu mji wa Tiro, nao utarudia kufanya uzinzi kwa kujiuza kwa mataifa yote ya dunia.
18 Fedha utakayopata itawekwa wakfu kwa Mwenyezi-Mungu. Mji wenyewe hautafaidika kwa fedha hiyo ila wale wanaomwabudu Mwenyezi-Mungu wataitumia kununulia chakula kingi na mavazi mazuri.