9 Ni Mwenyezi-Mungu wa majeshi!Yeye ndiye aliyeyapanga haya yote.Alifanya hivyo akiharibu kiburi chaona kuwaaibisha waheshimiwa wake.
10 Limeni sasa ardhi yenu enyi wakazi wa Tarshishi;maana hamna tena bandari kwa ajili ya meli kubwa.
11 Mwenyezi-Mungu ameunyosha mkono wake juu ya bahari,amezitetemesha falme;ametoa amri kuziharibu ngome za Kanaani.
12 Alisema: “Ewe binti Sidonihutaweza kufanya sherehe tena;hata ukikimbilia Kupro,huko nako hutapata pumziko!”
13 (Ni Wakaldayo, wala si Waashuru, waliowaacha wanyama wa porini wauvamie mji wa Tiro. Wao ndio waliouzungushia mji huo minara ya kuushambulia, wakayabomoa majumba yake na kuufanya magofu.)
14 Pigeni yowe enyi meli za Tarshishi,maana kimbilio lenu limeharibiwa.
15 Hapo mji wa Tiro utasahaulika kwa muda wa miaka sabini, muda wa maisha ya mfalme. Baada ya miaka hiyo sabini, mji wa Tiro utakumbwa na kile watu wanachoimba juu ya malaya: