16 Tunasikia nyimbo za sifa kutoka miisho ya dunia,nyimbo za kumsifu Mungu aliye mwadilifu.Lakini mimi ninanyongonyea,naam, ninanyongonyea.Ole wangu mimi!Wasaliti wanaendelea kuwa wasaliti,usaliti wao unazidi kuwa mbaya zaidi.
17 Hofu, mashimo na mitego,hivi ndivyo vinavyowangojeni enyi wakazi wa dunia.
18 Atakayeikimbia hofu atatumbukia shimoni;atakayetoka shimoni atanaswa mtegoni.Madirisha ya mbinguni yamefunguliwa,misingi ya dunia inatikisika.
19 Dunia inavunjikavunjika,inapasuka na kutikiswatikiswa.
20 Inapepesuka kama mlevi,inayumbayumba kama kibanda.Imelemewa na mzigo wa dhambi zakenayo itaanguka wala haitainuka tena.
21 Siku ile Mwenyezi-Mungu ataliadhibu jeshi la anganikadhalika na wafalme wa duniani.
22 Wote watakusanywa kama wafungwa shimoni;watafungwa gerezani pamoja kwa miaka mingi,na baada ya muda huo atawaadhibu.