1 Mwenyezi-Mungu asema hivi juu ya Koreshi:“Wewe ni mfalme wangu niliyekuteua;mimi naitegemeza nguvu yakoili uyashinde mataifa mbele yako,na kuzivunja nguvu za wafalme.Mimi nayafungua malango ya mji mbele yako,na hakuna lango litakalofungwa.
2 Mimi nitakutangulia,na kuisawazisha milima mbele yako.Nitaivunjavunja milango ya shaba,na kuvikatakata vizuizi vyake vya chuma.
3 Nitakupa hazina zilizofichwa gizani,na mali iliyo mahali pa siri,upate kutambua kwamba mimi ndimi Mwenyezi-Mungu,Mungu wa Israeli, ninayekuita kwa jina lako.
4 Kwa ajili ya mtumishi wangu Yakobo,naam, kwa ajili ya mteule wangu Israeli,nimekuita kwa jina lako;nimekupa jina la heshima ingawa wewe hunijui.