1 Nisikilizeni, enyi nchi za mbali,tegeni sikio, enyi watu wa mbali!Mwenyezi-Mungu aliniita kabla sijazaliwa,alitaja jina langu nikiwa tumboni mwa mama yangu.
2 Aliyapa ukali maneno yangu kama upanga mkali,alinificha katika kivuli cha mkono wake;aliufanya ujumbe wangu mkali kama ncha ya mshale,akanificha katika podo lake.
3 Aliniambia, “Wewe ni mtumishi wangu;kwako, Israeli, watu watanitukuza.”
4 Lakini mimi nikafikiri,“Nimeshughulika bure,nimetumia nguvu zangu bure kabisa.”Hata hivyo, Mwenyezi-Mungu atanipa haki yangu;tuzo la kazi yangu liko kwa Mungu.
5 Lakini asema sasa Mwenyezi-Mungu,ambaye aliniita tangu tumboni mwa mama yanguili nipate kuwa mtumishi wake;nilirudishe taifa la Yakobo kwake,niwakusanye wazawa wa Israeli kwake.Mwenyezi-Mungu amenijalia heshima mbele yake.Mungu wangu amekuwa ndiye nguvu yangu.
6 Yeye asema: “Haitoshi tu wewe kuwa mtumishi wangu,uyainue makabila ya Yakobo,na kurekebisha watu wa Israeli waliobaki.Nitakufanya uwe mwanga wa mataifa,niwaletee wokovu watu wote duniani.”
7 Mwenyezi-Mungu, Mkombozi na Mtakatifu wa Israeli,amwambia hivi yule anayedharauliwa mno,yule anayechukiwa na mataifa,na ambaye ni mtumishi wa watawala:“Wafalme watakuona nao watasimama kwa heshima,naam, wakuu watainama na kukusujudiakwa sababu yangu mimi Mwenyezi-Munguambaye hutimiza ahadi zangu;kwa sababu yangu mimi Mtakatifu wa Israeliambaye nimekuteua wewe.”