7 Naam! Shamba la mizabibu la Mwenyezi-Mungu wa majeshini jumuiya ya Waisraeli,na mizabibu mizuri aliyoipanda ni watu wa Yuda.Yeye alitazamia watende haki,badala yake wakafanya mauaji;alitazamia uadilifu,badala yake wakasababisha kilio!
8 Ole wao wanaonunua nyumba baada ya nyumba,wanaoongeza mashamba juu ya mashamba yao,mpaka kila sehemu inakuwa mali yao,na hamna nafasi kwa wengine nchini.
9 Nimemsikia Mwenyezi-Mungu wa majeshi akitamka hivi:“Hakika nyumba nyingi zitabaki tupu,majumba makubwa mazuri bila wakazi.
10 Shamba la mizabibu la eka kumilitatoa lita nane tu za divai;anayepanda kilo 100 za mbeguatavuna kilo 10 tu za nafaka.”
11 Ole wao wanaoamka asubuhi na mapemawapate kukimbilia kunywa kileo;wanaokesha hata usiku,mpaka divai iwaleweshe!
12 Katika karamu zao, hapakosekani vinubi,zeze, matari, filimbi na divai.Lakini hawajali matendo ya Mwenyezi-Mungu,wala kuzitambua kazi za mikono yake.
13 Kwa hiyo, watu wangu watapelekwa uhamishonikwa sababu ya utovu wao wa akili.Watu wenu mashuhuri watakufa njaa,watu wengi watakufa kwa kiu.