7 Nilikuacha kwa muda mfupi tu;kwa huruma nyingi, nitakurudisha.
8 Kwa hasira nyingi nilikuficha uso wangu kwa kitambo,lakini kwa fadhili za milele nitakuonea huruma.Mimi Mwenyezi-Mungu Mkombozi wako, nimesema.
9 “Nitafanya kama nilivyofanya wakati wa Noa:Wakati ule niliapa kwambasitaifunika tena ardhi kwa gharika.Basi sasa naapa kwamba sitakukasirikia tenawala sitakukemea tena.
10 Milima yaweza kutoweka,vilima vyaweza kuondolewa,lakini fadhili zangu hazitakuondoka,agano langu la amani halitaondolewa.Mimi Mwenyezi-Mungu nikuhurumiaye nimesema.
11 “Ewe Yerusalemu uliyeteseka,uliyetaabishwa na kukosa wa kukufariji!Nitakujenga upya kwa mawe ya thamani,misingi yako itakuwa ya johari ya rangi ya samawati.
12 Minara yako nitaijenga kwa mawe ya akiki,malango yako kwa almasi,na ukuta wako kwa mawe ya thamani.
13 “Watu wako watafunzwa nami Mwenyezi-Mungu,wanao watapata ustawi mwingi.