15 Ututazame kutoka mbinguni ee Mungu, uone,utuangalie kutoka makao yako matakatifu na matukufu.Iko wapi bidii yako kwa ajili yetu na nguvu yako?Usiache kutuonesha upendo wako.
16 Maana wewe ndiwe Baba yetu;Abrahamu, mzee wetu, hatujali,naye Israeli hatutambui;lakini wewe, ee Mwenyezi-Mungu, ni Baba yetu.Wewe umeitwa tangu kale: “Mkombozi wetu.”
17 Ee Mwenyezi-Mungu, mbona unatukosesha njia zako?Mbona unatufanya kuwa wakaidi hata tusikuogope?Rudi ee Mungu kwa ajili ya watumishi wako,makabila ambayo daima yalikuwa mali yako.
18 Kwa kitambo tu sisi watakatifu wako tulimiliki nchi,lakini maadui zetu wakaja wakaharibu maskani yako.
19 Tumekuwa kama watu ambao hujawatawala kamwe,kama watu ambao hawakujulikana kwa jina lako.