22 Bwana Mungu asema hivi:“Nitayapungia mkono mataifa;naam, nitayapa ishara,nayo yatawabeba watoto wenu wa kiume,kadhalika na watoto wenu wa kikena kuwarudisha kwako.
23 Wafalme watakushughulikia,na malkia watakutengenezea chakula.Watakusujudia na kukupa heshima,na kuramba vumbi iliyo miguuni pako.Hapo utatambua kuwa mimi ni Mwenyezi-Mungu;wote wanaonitegemea hawataaibika.”
24 Watu wa Yerusalemu walalamika:“Je, shujaa aweza kunyanganywa nyara zake?Au mateka wa mtu katili waweza kuokolewa?”
25 Mwenyezi-Mungu ajibu:“Naam! Hata nyara za shujaa zitachukuliwa,mateka wa mtu katili wataokolewa.Mimi mwenyewe nitawakabili maadui zako,mimi mwenyewe nitawaokoa watoto wako.
26 Nitawafanya wanaokukandamiza watafunane;watalewa damu yao wenyewe kama divai.Hapo binadamu wote watatambua kwambamimi ni Mwenyezi-Mungu, Mwokozi wako,mimi ni Mkombozi wako, Mwenye Nguvu wa Yakobo.”