2 “Nilipokuja kwa nini sikukuta mtu?Nilipoita mbona hamkuitikia?Je, mkono wangu ni mfupi nisiweze kuwaokoeni?Je, sina nguvu ya kuwakomboa?Tazama! Kwa kuikemea kidogo bahari hukauka,na mito nikaifanya kuwa jangwa,samaki wake wakafa na kunuka kwa kukosa maji.
3 Mimi hulivika anga giza,na kulivalisha vazi la kuomboleza.”
4 Bwana Mungu amenipa ufasaha wa lugha,niwatie moyo wale waliochoka.Kila asubuhi hunipa hamuya kusikiliza anayotaka kunifunza.
5 Bwana Mungu amenifanya msikivu,nami sikuwa mkaidiwala kugeuka mbali naye.
6 Mgongo wangu niliwaachia walionipiga,mashavu yangu waliozingoa ndevu zangu;walioniaibisha na kunitemea mate,sikujificha mbali nao.
7 Bwana Mungu hunisaidia,kwa hiyo siwezi kufadhaika.Uso wangu nimeukaza kama jiwe;najua kwamba sitaaibishwa.
8 Mtetezi wangu yuko karibu.Ni nani atakayepingana nami?Na aje tusimame mahakamani.Adui yangu ni nani?Na ajitokeze mbele basi.