8 Namweka Mwenyezi-Mungu mbele yangu daima;yuko pamoja nami, wala sitatikisika.
9 Kwa hiyo nitafurahi kwa moyo wote na kushangilia,nami nitakaa salama salimini.
10 Naam wewe hutaiacha nafsi yangu kuzimu,hutaniacha mimi mwaminifu wako nipate kuoza.
11 Wanionesha njia ya kufikia uhai;kuwako kwako kwanijaza furaha kamili,katika mkono wako wa nguvu mna mema ya milele.