Zaburi 42 BHN

KITABU CHA PILI

Sala ya MkimbiziZaburi 42 na 43 bila shaka zilikuwa wimbo mmoja hapo awali kama inavyoonekana dhahiri katika marudio ya aya ya 6 Zab 42 katika aya ya 11 na katika Zab 43 aya ya 5.

(Kwa Mwimbishaji. Utenzi wa Wakorahi)

1 Kama paa atamanivyo maji ya kijito,ndivyo ninavyokutamani, ee Mungu wangu!

2 Naona kiu ya Mungu, kiu ya Mungu aliye hai.Nitafika lini kwake na kuuona uso wake?

3 Machozi yamekuwa chakula changu mchana na usiku,waliponiambia kila siku: “Yuko wapi Mungu Wako!”

4 Nakumbuka tena mambo hayakwa majonzi moyoni mwangu:Jinsi nilivyokwenda na umati wa watu,nikawaongoza kwenda nyumbani kwa Munguwakipiga vigelegele vya shukrani;umati wa watu wakifanya sherehe!

5 Mbona nasononeka hivyo moyoni?Kwa nini nahangaika hivyo ndani mwangu?Nitamtumainia Mungu,maana nitamsifu tenayeye aliye msaada wangu na Mungu wangu.

6 Nimesongwa na huzuni moyoni mwangu,kwa hiyo ninakukumbuka wewe, ee Mungu,kutoka katika eneo la Yordani,kutoka mlima Hermoni na Mizari.

7 Nimeporomoshewa mafuriko ya majimafuriko ya maji yaja karibunayo yaita maporomoko mapya.Mawimbi na mapigo yako yamenikumba.

8 Mwenyezi-Mungu atanijalia fadhili zake mchana;nami nimwimbie wimbo wa sifa usiku,nimwombe Mungu anipaye uhai.

9 Namwambia Mungu, mwamba wangu:“Kwa nini umenisahau?Yanini niende huko na huko nikiombolezakwa kudhulumiwa na adui yangu?”

10 Nimepondwa kwa matukano yao,wanaponiuliza kila siku:“Yuko wapi, Mungu wako!”

11 Mbona nasononeka hivyo moyoni?Kwa nini nahangaika hivyo?Nitamtumainia Mungu,maana nitamsifu tena Mungu,aliye msaada wangu na Mungu wangu.