21 Maana nimefuata njia za Mwenyezi-Mungu,wala sikujitenga na Mungu wangu kwa uovu.
22 Nimeshika maagizo yake yote,sikuacha kufuata masharti yake.
23 Mbele yake sikuwa na hatia;nimejikinga nisiwe na hatia.
24 Mwenyezi-Mungu amenituza kadiri ya uadilifu wangu;yeye ajua kwamba mikono yangu haina hatia.
25 Wewe ni mwaminifu kwa walio waaminifu;mwema kwa wale walio wema.
26 Wewe ni mkamilifu kwa walio wakamilifu;lakini mkatili kwa watu walio waovu.
27 Wewe wawaokoa walio wanyenyekevu,lakini wenye majivuno huwaporomosha.